ILI MAHUSIANO AMA NDOA ILETE FURAHA INAHITAJIKA AMANI💯


Hakuna vipeuo wala unyambulishaji Kwenye Mahusiano/ndoa ila lililo kuu ni AMANI📍
Hata upendwe kiasi gani ama utimiziwe mahitaji kiasi cha kusaza kama huna AMANI ni Sawa na bure, Ni hasara kumkumbatia Mtu ambaye wewe kwa moyo wako unampenda sana ila yeye sio sababu ya AMANI YAKO🤔
Kuna faida kubwa kwa Mtu anayepewa AMANI na mtu ambaye hampendi💯
Kwa sababu hiyo hakuna sababu ya kusubiri UPENDO ila unatakiwa uuishi UPENDO.
Huwezi kuwa na AMANI kama hitaji lako halijatimia, Na watu wengi tunalazimisha AMANI huku tukijua mahali tulipo si sababu ya AMANI yetu etiiii kisa tu:-
👉 TUNAPENDA.
Kupenda ni jambo moja na kuwa na AMANI ndilo jambo gumu zaidi, Maana sio kila UNAYEMPENDA ATAKUPA AMANI pengine wewe si Mtu ambaye alikutarajia kuwa nae ila ikatokea tu.
Huwezi kupewa AMANI na mtu ambaye yeye mwenyewe HAKUPENDI ila ni rahisi kupewa AMANI tena ya hakika na ya kudumu na Mtu ambaye wewe humpendi ila yeye ANAKUPENDA💯
Kaa tafakari kisha chagua upande ambao wewe ndilo hitaji lako, Kuna wasopenda AMANI japo wanaumia kwa wanayopitia, na wengine wao kuitaka AMANI lakini hawawezi kuifuta iliko mwisho wao ni KUBAKIA NJIA PANDA😂
Huwezi kumuacha lakini ANAAKUUMIZA hata unaamua KUMSALITI huku ukiamini bado unamhitaji💃💃
#Elista_kasema_ila_sio_Sheria 🔨


(WAKUBWA TU 18+) JIFUNZE UFUNDI NA UTUNDU KATIKA MAPENZI UBORESHE MAHUSIANO YAKO PAKUA APP YA UFUNDI CHUMBANI , BONYEZA HAPA KUIDOWNLOAD KWENYE SIMU YAKO

No comments:

Theme images by imagedepotpro. Powered by Blogger.