CHOMBEZO:MPANGAJI EPISODE:12 (inaendelea..)






Yule mkubwa alikuwa na weupe wa asili,weupe ambao kwangu ulikuwa ni silaha tosha ya kunifanya nidondoshe kila kitu nilichonacho na kumuachia yeye. Usoni alikuwa kabeba macho legevu na ya uviringo kama ya samaki lakini yenye ukubwa fulani hivi wa bashasha. Nashindwa kuyaelezea,ila kama unataka kuyapata yalikuwaje,mwangalie Ray C.
Tuache macho,ee bwana sijawahi kumsifia mwanamke hadi shingo,ila yule bwana alikuwa ni kiboko wa yote. Ile shingo ilikuwa haina michirizi wala nini,halafu imetoka kwenda juu kidogo na baadae ikarembwa na kicheni cha silva yenye herufi ya F.
Sasa pale kati sasa,mitaa ya kifua,ohooo,nyie acheni masela,tena acheni kabisa,mwnaume nilishikwa na uchu wa ngono kama nimekula juisi ya pweza,au supu ya pweza kama hujanielewa.
Kifua kilikuwa kimebetuka kwa juu,na kubeba mtindi wa maana,yaani umevimba na kutanuka. Nilidhani labda kayapiga jeki,lakini nilivyomzoea,niligundua hakuwa mzee wa jeki,kitu kilikuwa orijino kutoka kwa mpendwa MUNGU. Hiyo ni mitaa ya kifuani,ngoja niishie hapo,halafu baadae nitarudi kummalizia pale aliposimama.

Sasa yule mdogo wake wa kati. Yeye alikuwa hana tofauti sana dada yake,nasema ni dada yake kwa sababu walifanana,yaani kwa kuwaangalia tu! Huwezi kukataa hili nalokwambia.
Walikuwa wanafanana sana,lakini tofauti yao ni huyu mdogo kuwa na macho ambayo yaliregea zaidi ya dada yake.Huyu dada yake alikuwa na macho regevu lakini yalikuwa yamekaza,ila huyu mdogo alikuwa anarembua bwana,yaani sijui akipata mafua au malaria inakuwaje yale macho. Tukiacha hilo,huyu mdogo alikuwa pia na chuchu konzi,yaani titi jembamba halafu limechongoka kwenda mbele kama ncha ya mshale. Nani asitamani mazaga kama hayo,kwanza nilipiga na magoti kimoyomoyo na kumshukuru maulana kwa kunileta jiji la Arusha.
“Mbona umesimama mlangoni?”.Sauti ya yule dada mkubwa ilinitoa katika ule mshangao wangu na kunirudisha duniani.
“Mimi sikujua kama hapa ni jikoni. Siwezi kukaa humu”.Nilimjibu huku bado nikiwa naendelea kumtathimini yule binti aliyeumbika kupita malaika wa shetani.
“Ahaa,pole aisee. Karibu Arusha bwana”.Dada yule aliendeleza maongezi.
“Asante aisee. Naona kuna baridi kama nipo Antakatika”.Na mimi nikajibu na kuingiza kiusomi changu cha kuzugia.
“Ha ha haaa. Tulikuona ulivyokimbilia ndani,mbona kuna joto sasa hivi?”.Alijibu huku akitabasamu na kunipa moyo kuwa kuna joto wakati mimi nilikuwa nahisi naweza kuganda muda wowote.
“Wewe,masikhara hayo. Huu ubaridi unaingia hadi kwenye kucha,halafu wewe unasema kuna joto”.Nilimjibu kwa kupingana naye.
“Utazoea tu! We Sheila,mpe stuli mgeni akae”.Binti yule akamwambia yule mdogo wake wa kati anipe stuli nikae maana tayari alishaanza kunogewa na sauti ya gharama kutoka kwa Prince Mukuru.
“Aaag. Mwache akae bwana,mimi wala si wa kukaa hapa. Sijui mzee yupo?Maana niliongea naye asubuhi sana kisha nikarudi kulala”.
“Baba yupo sebuleni,twende nikupeleke maana ni wewe ndiye alikuwa anakusubiria ili aende mihangaikoni kwake”.Alijibu yule binti na kutoka nje,kisha akatangulia mbele kwenda ilipo nyumba yao.
Alikuwa kavaa khanga kiheshima kabisa,lakini bado umbo lake ambalo lilijengwa kwa makalio madogo na ya kichokozi,lilionekana vema kwa mvuto na kwa hamasa ya kila mwanaume kutaka kuona kilichofichika ndani ya nguo ile aliyovaa. Sikuona miguu yake kwa sababu khanga aliishusha hadi chini.
“Karibu kaka”.Nilikaribishwa na yule binti,na mimi nikavua sendro nilizokuwa nimevaa na kubaki na soksi. Nikaingia ndani na kumkuta yule mzee akiwa katika mavazi ya kichungaji. Nikamsalimia kwa heshima zote,na baadae aliniomba nikae kwenye kochi moja lililopembeni ya nyumba ile. Nikatii ombi lake kwa kukaa,na kisha nikatega sikio kumsikiliza mzee yule.
“Umesema unaitwa Prince eeh”.Alianza yule mzee kwa kujikumbusha jina langu,wakati huo yule binti alikuwa hayupo,kishatoka nje.
“Ndiyo Mzee,naitwa Prince Mukuru”.Nilimjibu kwa ufasaha zaidi.
“Sawa Prince,karibu sana Arusha na karibu sana nyumbani kwangu. Sasa nataka nikutambulishe kwa familia yangu ili ujuane nao,na wakija watu tofauti na hawa,basi uweze kuwauliza wanataka nini,maana kuna wezi sana hapa jijini”.Mzee yule aliongea huku kakunja nne ndani ya kanzu yake ya kichungaji.
“We Faridaa”.Aliita mzee yule.
“Abee”.Ikaitika sauti ya yule binti mkubwa.
“Njoo na wenzako”.Akaamrisha mzee kwa sauti ileile.
Baada ya dakika kadhaa,wale mabinti walikuwa kwenye kochi kubwa lile la watu watatu.
“Huyu ni mgeni,ni mdogo wake George,katoka Dar. Kafika hapa jana usiku wa saa tatu. Anaitwa Prince”.Mzee yule akanitambulisha kwa wanawe ambao mimi nilishaanza kupiga nao stori kidogo kidogo.
“Karibu Prince”.Nikakaribishwa na mabinti wale kwa wao kupokezana kusema karibu Prince.
“Ehee. Prince. Hawa ni wanangu,huyu mkubwa anaitwa Farida Donyo,huyu anaemfata anaitwa Sheila naye ni Donyo na huyu wa mwisho anaitwa Lilian.

****

:: Hatimaye Prince anakabidhiwa tena bucha? je ataambulia hata mmoja? itakuwaje?

:: Usikose Episode ya 13........stay updated..





(WAKUBWA TU 18+) JIFUNZE UFUNDI NA UTUNDU KATIKA MAPENZI UBORESHE MAHUSIANO YAKO PAKUA APP YA UFUNDI CHUMBANI , BONYEZA HAPA KUIDOWNLOAD KWENYE SIMU YAKO

No comments:

Theme images by imagedepotpro. Powered by Blogger.