Simulizi: Mateso ya maisha yangu.




Nakumbuka mnamo mwaka 2012 mume wangu kipenzi alifikwa na umauti akiwa kazini kwake, ambapo kazi yake kubwa ilikuwa ni kupasua mbao.

Siku hiyo nikiwa sina hili wa lile muda wa kama saa tisa alasiri, niliisikia simu yangu ikiita, niliichukua simu ili kutazama ni nani aliyekuwa ananipigia kwa wakati huo, ila namba ilikuwa ngeni katika simu yangu.

………..Nilibonyeza kitufe cha kupokelea simu

Hallo.... mimi ndiye niliyeanza kusema

………..Hallo... nilisikia sauti ya mwaume.

Shemeji, habari yako ilikuwa ni sauti ya mwanaume yule.

Salama nilijibu,

………..Samahani nani mwenzangu, Ni mimi shemeji yako Yuzo.

Oooh shem yuzo kwema? nilihoji.

Kwema kiasi ilikuwa ni sauti ya shem yuzo, moyo wangu ilishtuka, 

kunani tena shem yuzo, sikusita kuhoji kwani shem yuzo nilikuwa namfahamu fika alikuwa ni rafiki mkubwa wa mume wangu, 

Shem aliendelea kuzungumza huku akiwa amejawa  na simanzi nyingi ndani ya sauti yake,

Samahani shem, najua sina budi kukupa taarifa hizi ijapokuwa ni ngumu kuamini, aliweke pozi kidogo kisha akaendelea.

Mumeo kwa bahati mbaya wakati tunafanya kazi zetu hizi za kila siku amedondokewa na gogo hivyo amefariki.

mmmmmh, niliguna huku nikiwa siamini kile ambacho nimekisikia, 

shem imekuwaje, sikusita kuhoji huku sauti yangu na machozi yangu navyo vikiwa havipo mbali nami.

Ni story ndefu shem wangu ila jambo muhimu la kufanya  kwa sasa ni kuwaambia wazazi wake pamoja na ndugu na jamaa wa karibu kuhusu msiba huu, mengineyo tutakuja kuongea kisha akataa simu.

Kiukweli zilikuwa ni taarifa ngumu sana kwangu kuzipokea kwa mikono miwili kwani nilihisi zinanielemea, nililia sana na nilifanya kama ambavyo shem yuzo alivyoniagiza.
**********
Kwa kuwa mwili wa mume wangu ulikuwa umeharibika sana kutokana na ajali aliyokuwa ameipata, hatukuchukua muda mrefu kufanya maziko.

Namshukuru Mungu wangu, maziko yalifanyika salama……. Ila
Kiukweli baada ya maziko maisha yangu yalianza kubadilika  na kuwa  magumu sana kupita kiasi, ndugu zangu wote walitenga nami, pamoja na familia yangu kiujumla.

Sikujua ni nini kimesababisha mpaka ndugu zangu kuwa vile, ila baada ya kufanya uchunguzi ni kwanini ndugu wameamua kunifanyia vile, nilikuja kugundua kwamba walifanya vile kwani waliamini na waliaminishana mimi nimemtoa kafala mume wangu kwani kabla ya kupatwa na umati tulikuwa na migorogoro ya hapa na pale katika maisha yatu,

Japo ukweli ni kwamba mimi sikuhusika na hayo waliyoyasema  hata kidogo, pia ukweli ni kwamba mimi na Mungu wangu ninayemuamini ndiye anajua ukweli wote.

Ikiwa mchana, ikiwa giza…. Maisha yangu na famili yangu yalizidi kuwa magumu sana kila jua lilipokuwa linachomoza, kila kukicha nilionja uchungu wa maisha, kuna wakati nilikuwa natafakari hivi kwanini Mimi? Kiukweli nisiwe Muongo maisha yalikuwa ni magumu sana kupita kiasi.

 Pia ikumbukwe kwa wakati huo nilikuwa na watoto watatu, mkubwa alikuwa darasa tano, mtoto wa pili alikuwa darasa la pili  ila huyu wa tatu alikuwa ni mdogo sana, ndiyo kwanza alikuwa na miezi mitatu pekee.
*********
Kula kwangu pamoja na familia yangu kulikuwa ni kugumu sana, kuna wakati nilitamani hata kulitumikia vyema kabila langu la uhehe kwa kujinyonga, ila kadri nikiwataza wanangu mawazo hayo machafu yalikuwa yakijitenga nami.

Katika siku ambazo huwa huwa siisahau ni tarehe 8. 10 2016, siku  hiyo nilibahatika kufanya kazi kwa mama mmoja ya kumfulia nguo zake, nilifanya vile kwani pesa aliyokuwa ananilipa ilinisaidia kuhakikisha mkono wangu na mikono ya wanagu inakwenda kinywani.

Mara baada ya kupata ujira wangu kutoka kwa mama yule nilinunua unga nusu kwa ajili ya kupika chakula cha mchana. Nilipika chakula kile japo kilikuwa ni chakula kidogo. Kwa kuwa msemo wa wahenga unasema ni heri mzazi abaki njaa ila wanao wale, hivyo niliungana kwa kiasi fulani na wahenga hao.

Kwa kuhakikisha nakula  kidogo ili wanangu wasijisikie vibaya, Nilikula kidogo wao nikawaacha wanakula kisha mimi nikaelekea nje kwenda kumuogesha mtoto wangu mdogo wa miezi mitatu.

Wakati nikiwa nje namuogesha mtoto wangu mdogo, nilisikia watoto wangu wale wawili ndani wakigombana, ugomvi wao ulitokana na kutoshiba chakula kwa sababu siku hiyo chakula kilikuwa ni kidogo kama ambavyo nimesema hapo awali. Ni dhairi hawakushiba.

Kutokana na ugomvi wao kuendelea kuwa mkubwa, nilimuacha mtoto mdogo ndani  beseni lilokuwa lina maji na kukimbia ndani kwenda kuamua ugomvi wa wanangu. Sikumuacha mtoto mdogo makusudi ila nilikuwa kama nimechanganyikiwa.

ile nafika tu ndani nakuta mtoto wangu mwingine ameshika kisu amekwisha mchoma mtoto mwingine kwani walikuwa wanagombania sufuria ambayo niliipikia chakula. Yule aliyemchoma akaanza kukimbia kuelekea nje, nami nikiwa katika hasira nilianza kumfukuza kuelekea barabarani ambapo alipokuwa anakimbilia.

Ile anafika barabarani kwa bahati mbaya naye akagongwa na gari na kufariki pale pale, ikumbukwe wakati huo mtoto mdogo nilikuwa nimemuacha kwenye peseni naye alifariki kwa kuwa alikunywa maji niliyokuwa nayatumia kumuogesha.

Kiukweli hapa nilipo mawazo yangu yamepupazwa, sielewi moja wala mbili nimeipoteza familia yangu yote kwa muda mfupi, Sielewi ni nini cha kufanya, maisha yamekuwa ni mtihani usiyo na majibu sahihi kwangu, naomba japo ushauri wako uweze fariji moyo wangu, kwani haya ni mateso ya maisha.

Mtunzi; Benson Chonya

bensonchonya23@gmail.com 


(WAKUBWA TU 18+) JIFUNZE UFUNDI NA UTUNDU KATIKA MAPENZI UBORESHE MAHUSIANO YAKO PAKUA APP YA UFUNDI CHUMBANI , BONYEZA HAPA KUIDOWNLOAD KWENYE SIMU YAKO

No comments:

Theme images by imagedepotpro. Powered by Blogger.