KAMA UNA MOYO MWEPESI USISOME STORY HII,WENGI WAMELIA SANA !!




Nilipofika nyumbani usiku ule, mke wangu

aliponitayarishia chakula, nilimshika mkono na

kumwambia, Kuna kitu nataka nikwambie. Mke wangu

alikaa chini na kula chakula kimya akiwa tayari

kunisikiliza. Tena nikagundua macho yake yalionyesha

anaumizwa. Nilishindwa hata namna ya kuanza

kufumbua kinywa changu. Lakini ilibidi nimwambie ili

ajue nilikuwa nikifikiri nini juu yake.

Nataka kukupa talaka. Nilianza kusema kwa utulivu.

Alionekana kutokereka na maneno yangu badala yake

aliniuliza kwa sauti ya upole ‘kwa nini?’ Sikumjibu swali

lake. Kutojibu kulimfanya akasirike. Akatupa kijiko na

akanikaripia, ‘wewe si mwanamume!’ Usiku ule,

hakukuwa na maongezi kati yetu. Alikuwa akilia kwa

kwikwi. Nilifahamu kwamba alitaka kujua ni nini

kimetokea kwenye ndoa yetu. Lakini kwa hakika

nisingeweza kumpa jibu wala sababu ya kuridhisha;

alionekana si mali kitu kwangu penzi langu lilihamia

kwa Mary. Sikumpenda tena mke wangu mawazo yote

yalikuwa kwa Mary. Kwa kweli nilimdharau mke wangu!

Huku moyo wangu ukijua wazi kwamba nafanya kosa,

niliandika talaka ambayo ilionyesha kwamba yeye (mke

wangu) angepata nyumba yetu, gari na atakuwa na hisa

30% ya kampuni yetu. Aliangalia talaka ile na kuichana

vipande vipande.

Mke ambaye tumeishi nami kwa miaka 10 alionekana

mgeni machoni mwangu. Nilimuonea huruma kwa

muda, rasilimali na nguvu alizopoteza lakini sikuweza

kurudi nyuma kwa sababu Mary aliuteka moyo wangu

kisawasawa. Hatimaye mke wangu alilia kwa sauti

mbele yangu, jambo ambalo kwa hakika nilitarajia.

Kwangu mimi kilio chake kilinipa nafuu.

Wazo la kuachana na mke wangu limenisumbua kwa

majuma kadhaa na sasa limeendelea kuimarika na kuwa

jambo la hakika zaidi.

Siku iliyofuata nilikuja nyumbani kwa kuchelewa sana

nikakuta mke wangu akiandika jambo mezani.

Sikutamani hata kula chakula alichonipikia nilikwenda

moja kwa moja chumbani na usingizi ulinichukua mara

moja kwa sababu nilikuwa nimechoka baada ya kula

raha za kufa mtu na Mary

Usiku nilishtuka usingizini mke wangu alikuwa bado

akiandika. Sikujali kabisa nikajifunika vyema shuka na

kulala tena. Asubuhi yake alinikabidhi masharti ya

talaka yake: hakutaka kitu chochote kutoka kwangu

lakini alihitaji apate angalau mwezi mmoja wa

kujiandaa kabla hajaachika. Akaomba kwamba katika

kipindi hicho cha mwezi mmoja sote mimi na yeye

tujitahidi kuishi maisha ya upendo au kawaida kwa

kadiri itakavyowezekana. Sababu yake ilikuwa ndogo

lakini muhimu: mwanetu wa kiume alikuwa akikaribia

kufanya mtihani katika mwezi uliofuata kwa hiyo

hakupenda mtoto aathirike kisaikolojia kwa sababu ya

kuachana kwetu. Hili halikuwa tatizo kwangu, nilikubali

mpango wake. Lakini alikuwa na sharti la ziada,

aliniomba nikumbuke jinsi nilivyombeba siku za fungate

yetu hasa siku ya harusi yetu. Akaniomba na kunisihi

kwamba katika kipindi hicho cha mwezi mmoja niwe

nambeba kutoka kitandani kwetu mpaka mlango wa

kutokea kila asubuhi. Nilidhani anakaribia kuwa kichaa.

Ili kufanya siku zetu za mwisho zisiwe na migogoro

nilikubaliana na masharti yake ya ajabu.

Nilimsimulia Mary kuhusu masharti ya kuachana na

mke wangu. Mary alicheka sana, aliona ni ujinga. ‘Hata

akitumia ujanja wa namna gani talaka ni lazima’,

alisema Mary tena kwa dharau. Mimi na mke wangu

hatukuwahi kugusana tangu nilipomweleza dhamira ya

kumtaliki. Kwa hiyo nilipombeba kwa mara ya kwanza

sote tulinuniana. Mwanetu alifurahi sana na kupiga

makofi nyuma yetu, ‘aah baba kambeba mama

mikononi mwake’. Maneno yake yalinichoma moyoni

moja kwa moja. Kutoka chumbani kwetu hadi sebuleni,

halafu tena mpaka mlangoni, ni zaidi ya mita kumi

nimembeba mke wangu. Alifumba macho na kusema

kwa sauti laini na ya upole; usimwambie mwanetu juu

ya talaka. Nilikubali kwa kichwa, ingawa nilijisikia

vibaya. Nilimuweka chini nje ya nyumba.

Alienda kituoni kusubiri basi la kazini kwake nami

nikaendesha gari kwenda ofisini kwangu. Siku ya pili,

zoezi lilikuwa rahisi kwetu sote. Aliegemea kifuani

pangu. Nilisikia harufu nzuri ya uturi aliofukiza kwenye

blauzi yake. Nikagundua kwamba sijamuangalia kwa

makini mke wangu kwa kipindi kirefu sana. Nikagundua

hakuwa binti tena. Kulikuwa na mikunjo usoni na

nywele zake zilianza kuwa nyeupe! Ndoa yetu imekula

urembo wake. Kwa dakika moja nikafikiri kwa nini

namfanyia hivi.

Siku ya nne nilipombeba hisia za mapenzi kati yetu

zilirejea. Huyu ni mwanamke aliyejitoa kuishi nami na

tumeishi kwa miaka kumi sasa. Siku ya tano na ya sita

ilikuwa wazi kwamba mapenzi yetu yalikuwa yakimea

upya. Sikumwambia Mary kuhusu jambo hili. Kadiri

mwezi ulivyokaribia kwisha niliona raha kumbeba mke

wangu na zoezi likawa rahisi zaidi. Pengine kufanya

kazi hii kila siku kuliniimarisha zaidi.

Alikuwa akichagua nini cha kuvaa asubuhi. Alichagua

mavazi kadhaa hakupata linalomfaa. Kisha akaguna,

‘nguo zangu zote zimekuwa kubwa’. Nikagundua

kwamba mke wangu amepungua sana, nadhani ndiyo

maana niliweza kumbeba kirahisi. Ghafla jambo

likanichoma... mke wangu ana uchungu na maumivu

makuu moyoni mwake. Bila kujitambua nikamgusa

kichwa chake. Mara mtoto wetu akatokeza na kusema

‘baba ni wakati wa kumbeba mama muende kazini’.

Kwake kumuona baba akimbeba mama likawa ni jambo

la furaha sana. Mke wangu alimuonyesha ishara

mwanetu asogee karibu na akamkumbatia kwa upendo

mkuu. Niligeuza uso wangu nisije nikabadili mawazo

katika dakika ya mwisho. Kisha nikambeba mikononi

mwangu kutoka chumbani, sebuleni halafu mpaka

mlangoni. Mkono wake laini ulikuwa umeizunguka

shingo yangu kwa upendo. Nilimkumbatia mwili wake;

ilikuwa ni mithili ya siku ya ndoa yetu. Lakini wepesi

wake ulinitia mashaka.

Siku ya mwisho nilipombeba nilipata shida hata kupiga

hatua moja. Mtoto wetu alishakwenda shuleni.

Nilimshika kwa karibu na kumwambia sikubaini kwamba

maisha yetu yalikosa upendo. Nikaenda zangu ofisini….

Nikashuka garini hata bila kufunga mlango. Maana

nilihisi nikichelewa tu ninaweza kubadili nilichoamua....

nikapand ngazi. Mary alifungua mlango nikamwambia,

‘Samahani, Mary, sihitaji tena kumtaliki mke wangu’.

Akaniangalia kwa kustaajabu, halafu akagusa kichwa

changu. Akaniuliza ‘Unaumwa?’ Nikaondoa mkono wake

kichwani kwangu. ‘Samahani, Mary, nimesema sitaki

kumtaliki mke wangu. Nadhani ndoa yangu haikuwa na

furaha kwa sababu sikuthamini undani wa maisha yetu,

mimi na mke wangu, si kwamba hatupendani.

Nimetambua hilo tangu nilipombeba siku ya ndoa yetu

nilitakiwa kumbeba siku zote za maisha yetu,

nampenda mke wangu sitamuacha mpaka kifo

kitakapotutenganisha.’

Ikawa kama Mary alizinduka usingizini. Akanizaba kibao

cha nguvu, akajiegemeza mlangoni na kuanza kulia.

Nikashuka ngazi na kuondoka zangu. Nikaingia kwenye

duka la maua nikaagiza maua mengi mazuri kwa ajili

ya mke wangu. Muuzaji akaniuliza aandike nini kwenye

kadi. Nikatabasamu na kuandika “Nitakubeba kila

asubuhi mke wangu mpaka kifo kitakapotutenganisha”.

Jioni ile nilifika nyumbani na maua mikononi mwangu,

tabasamu kubwa usoni nikakimbia mpaka chumbani,

nikapokelewa na maiti ya mke wangu kitandani.

Kumbe mke wangu alikuwa akisumbuliwa na saratani

kwa miezi kadhaa nami nilishindwa kubaini kwa sababu

nilihamishia akili yangu kwa Mary. Alijua kwamba

angekufa karibuni na alitaka asiniingize katika chuki na

mwanetu kama ningelazimisha talaka mapema.

Angalau machoni mwa mwanangu naonekana ni mume

mwema.

Mungu nisaidie Nisifike huku mimi.

Kama Stori Hii Imekugusa Na Ungependa Marafiki Nao

Waisome Basi Unaweza kusambaza (share na wenzako)



(WAKUBWA TU 18+) JIFUNZE UFUNDI NA UTUNDU KATIKA MAPENZI UBORESHE MAHUSIANO YAKO PAKUA APP YA UFUNDI CHUMBANI , BONYEZA HAPA KUIDOWNLOAD KWENYE SIMU YAKO

No comments:

Theme images by imagedepotpro. Powered by Blogger.