Je mwanaume mwenye tabia hizi anafaa kua mume?



Napenda kuomba msaada wenu wa mawazo ili na mimi nipate ushauri wenye hekima. Nina rafikiangu alipata mchumba wakati yule kaka anamuomba dada huyo awe mchumba wake mungu akijalia wawe mke na mume dada alikataa akawa haamini   nikweli, lakini baada ya huyo kaka kumfwatilia kwa muda mrefu dada akaona the guy was serious akakubali then akamuomba wakapime kaka akakubali wakakutwa salama. 
mahusiano yameanza mpaka ndugu pandezote mbili wakajua imebaki wazazi kutambulishwa, shida inakuja huyo kaka anaongea sana kupita kiasi yani wakikaa sehem yeye ndo aongee kupingwa hataki, chochote atakachokiona au kufanya lazima aseme, akinunua zawadi ya mchumba wake lazima rafiki wa dada huyo na wa kaka huyo watajua,  
kunawakati dada huyo aliumwa sana tumbo huyo kaka akamwambia ntakuijia home nikupele hosptl, dada alivopona anakutana na rafiki zake kaka huyo wanampa pole na kumwambia jamaa alitwambia uliumwa na ametumia pesa nyingi sana kukutibisha wakati haikua kweli, dada akanyamaza, akimtoa kwa dinner or lunch lazima dada huyo ataambiwa flani alisema juzu mlikua sehem kwa dinner huezi pata mwanaume anakupa good time hivo, anasahau kunamuda hakua vizuri dada huyo alimsaidia sana bila kulalamika pamoja nakua mwanaume anaumri mkubwa kuzidi msichana, 
akipata pesanyingi dada anamshauri nunua hata kiwanja jenga punguza kula life anamgombeza anamwambia mi ni msomi sana najua ninacho kifanya kwanza nipe muda ninamambo mengi, anapotea haonekani dada akaamua kuchukua makosa yeye na kumuomba msamaha ili tu abadilike ache kuongea kila kitu pia wapendane na wafanye maendeleo yao kwaajili ya future zao akasema sawa pia ntajirekebisha, baada ya siku dada anataniwa na rafiki wake na wamskaji nasikia ulimlilia jamaa unamuomba msamaha ili mpendane hiyo ika m put down sana huyo dada, na nimsichana anaejiheshi sana na anahofu ya mungu, kaka kaona mambo si mazuri na dada hana mpango tena au kapata matatizo anarudi kuomba msamaha 
sasa dada huyo kanishirikisha ni mshauri amtimue? Au amvumilie? Anauliza mtu wa hivyo anaweza kuwa mume mwema? Au nikukaribisha maumivu aibu na umaskini kuishi bila maendeleo, mimi nilimwambia aamuombe mungu ampe huyo kaka mtu mwingine ili yeye apewe na mungu mume mwema anaemstahili huyo hamfai na hawezi acha mdomo.wenye mawazo yenye kueleweka nisaidieni tumsaidie kijana mwenzetu jamani.


(WAKUBWA TU 18+) JIFUNZE UFUNDI NA UTUNDU KATIKA MAPENZI UBORESHE MAHUSIANO YAKO PAKUA APP YA UFUNDI CHUMBANI , BONYEZA HAPA KUIDOWNLOAD KWENYE SIMU YAKO

No comments:

Theme images by imagedepotpro. Powered by Blogger.