MUME WANGU ALIKUA AKINIFUNGIA NJE NA KUINGIA NA WANAWAKE WENGINE NDANI!



Mvua kubwa ilikua inanyesha, mimi nilikua nje nikinyeshewa na mwanangu mkononi, nilikua nimejibanza kwenye ukuta nikiigeuzia mgongo mvua huku nimemkumbatia mwanangu ili maji ya mvua yasimguse, mtoto wangu wa miezi sita alikua kalala, pamoja na baridi yote hiyo lakini alilala usingizi fofofo. Nilimshukuru Mungu kwa hilo kwani nilijua kuwa kama angelia basi majirani wangejua kilichokua kinaendelea na lingekua ni tatizo.

Mume wangu alikua ndani, alikuja siku hiyo na mwanamke mwingine, alikua ni binti mdogo tu na nilipoongea ndipo alinipiga na kunifukuza na mtoto, alinipiga sana nikaamua kutoka kutokana na mvua, walikua ndani wakifanya mapenzi, nilikaa nikijua kuwa ni lazima atakuja kuniita, mume wangu ni wale watu amabo huonekana kama walokole hivyo asingesubiri mpaka aubuhi.

Kweli kabla hakujapambazuka alitoka na yule binti, akamsindikiza na aliporudi alinifuata pale nilipokua nimesimama. “Ingia ndani au unataka watu wakuone ili wajue kama nakunyanaysa.” Aliniambia kwa suti ya upole, kwa kumuangalia usingefikiria kuwa jana yake ndiyo alitoka kunipiga na kunilaza nnje, bila kujibu chochote nilirudi ndani, nilimlaza mtoto na kuanza kusafisha nyumba wkani walichafua kila sehemu, baada ya kumaliza nilimuandalia nguo za kuvaa kazini, nikamuandalia chai alikunywa na kuondoka.

Masha yaliendelea, nilikua kwenye ndoa kwa miaka kumi na mume wangu, mwanzo wa ndoa yetu ulikua mzuri, alikua akinipenda na kunijali, lakini nilipopata ujauzito wa kwanza ulianza kunisumbuasumbua na kwakua nilikua napata kila kitu basi niliacha kazi na kuwa Mama wa nyumbani, lengo lilikua ni kufanya biashara lakini ilsihindikana, baada ya kuacha kazi mambo yualikua mengi, mara mtoto wa kwanza na wa pili ambao wote ni wakubwa wapo bweni wanasoma na akaja watatu huyu mdogo.

Mume wangu alibadilika akawa ni mtu wa kunipiga bila sababu, kuninyanyasa na kunitukana kila nikiomba kitu nimasimango, alianza kuabdilisha wanawake kama nguo, mwanzoni nilikua nikiulizia lakini napigwa, baada ya kuona habadiliki niliamua kukaa kimya. Alipoona nimekaa kimya alianza kuwaleta mpaka nyumbani, alikua akija nao wanafanya mapenzi chumbani mimi niko sebuleni kipindi nina mimba mpaka kuifungua.

Sikuweza kulalamika chochote kwani mbele za watu mimi ndiyo nilikua naonekana kama nina tatizo. Mume wangu ni wale watu wa kanisani kila siku, wale watu wa kutoa michango na kusaidia ndugu hivyo hata nilipolalamika kwa Mama yangu mzazi mimi ndiyo nilionekana kama nina matatizo siwezi kuvumilia ndoa. Kwakua sikua na pakwenda sikua na namna zaidi ya kuvumilia ingawa nilikua naumia.

Alikua akinitukana sana, ikafikia wakati hataki hata kufanya mapenzi na mimi, alikua hanigusi na kila nikijaruibu kumgus aananisukuma, ananiambia kuwa mimi ni mchafu hivyo anasikia kchefuchefu hata kunigusa, nilijitahidi kuoga, kuwa msafi na kufanya kila kitu ili kumvutia lakini aliniona kama takataka, hakunigusa wala kunijali, kitu pekee alichokua akijali ni wanae,. Waliwapeleka katika shule nzuri na huyu mdogo alikua anamnunulia kila kitu huku mimi akinitenga.

Mwaka jana mwishoni mume wangu alianza kubadilika, alianza kujirudi, wakati huo mwanangu wamwisho alikua na miaka miwili. Alianhza kunitaka kimapenzi na kutaka kurudiana, lakini mimi sikua katika mood, kuna kitu kilikua kinaniambia hapana, alianza kunilazimishia na kutaka kunibaka, nilijitahidi kujitoa mikonini mwake lakini alikua akinipiga sana na kuniambia kuwa mimi ni mke wake na ana haki ya kunifanya chochote.

Lakini bado nilisita, nisingeweza kumuamia mtu kitu, aliacha kuhudumia hata chakula cha mtoto akawa hatoi tena. Kwakua sikua na kazi nililazimika kumkubalia, tukawa tunashirikiana kimwili kama kawaida ingawa sikua nikisikia chochote, mume wangu alikua akifanya mapenzi kwa nguvu, hakua akiniandaa wala nini ni kama vile alikua ananikomoa kitu ambacho kiliniondoa kwenye mood na hivyo kumkasirisha nikaishia kupigwa tu.

Tukiwa katika kipindi hicho kuna shoga mmoja alikufa, alikua ni shoga maarufu mtaani na watu walisema kuwa kafariki kwa UKIMWI, sikujali kwani yalikua hayanihusu, lakini baada ya mazishi ndipo zilizuka tetesi kuwa kumbe mume wangu alikua akitembea naye kwa muda mrefu na huyo shoga kabla ya kufa alikua akitamba kuwa kuna watu kawaambukiza UKIMWI na mume wangu ni mmoja wapo. Nilishtuka sana na kuamua kwend akupima, nilipoma na kukuta niko salama.

Nilimuambia mume wangu ambaye alibisha na kuishia kunipiga akisema kuwa namdhalilisha. Lakini sikukubali nilimbana sana na kutishia kuondoka na kumuambia kila mtu, hapo ndiyo alikiri kweli alishakua na mahusiano na yule shoga na kweli kaambukizwa UKIMWI na ndiyo maana alirudi kwania likua katubu anataka kuwa na familia yake. Nilijikuta nalia tu nikiamini kuwa alikua anataka kuniambukiza kwa makusudi, kwa hasira nilimchukua mwanangu na kurudi kwetu.

Nilimuambia Mama kilichotokea lakinia linishangaa, aliniambia hata kama mume wangu kapata matatizo bado ni mume wangu na wakati huu ndiyo anahitaji faraja kutoka kwangu. aliniamba nimsamehe kwani ndiyo ndoa ni kuvumiliana katika shida na raha. Mimi nilikataa lakini Mama alinirudisha na kuniambia ili wanipokee mpaka nirudishwe na mume wangu, nilimuambia Baba yangu ambaye naye aliniambia hivyohivyo.

Hapo sikua na namna zaidi ya kurudi kwa mume wangu kwania likataa kuniacha kwa talaka na kwakua sikua na pakwenda basi sikua na namna. Nilirudi, mume wangu alikua mpole akiniambia kuwa tutakua tunatumia kinga kwani mimi ndiyo nitalea watoto kama akifarikidunia. Mimi nilimkubalia kwa shongi upande nikiwa na wasiwasi. Miezi miwili ya kwanza ilikua mizuri lakini baadaye alibadilika, siku moja alinipiga sana na kuniingilia kwa nguvu, alianza kuniingilia kinyume na maumbile.

Alifanya hivyo huku akinipiga na kunilaumu mimi akiniambia mimi ndiyo nimemsababishia kuambukizwa ukimwi kwani sikua mke bora kwake. Alinifanyia hivyo usiku kucha ana subuhi aliondoka na kuniacha nyumbani mwenyewe sina hili wala lile. Nilishindwa kuvumilia, nilimchukua mwanangu na kwenda kwa rafiki yangu mmoja, nilimuelezea kila kitu kwakua yeye alikua akiishi peke yake baada ya kufiwa na mume wake aliniruhusu kukaa kwake nikitafuta kazi.

Alinisaidia na mwezi uliopita nilipata kazi katika kampuni moja ya kuagiza magari nnje ya nchi. Maisha yalianza kwenda vizuri mwezi huu nikapanga chumba changu, mume wangu alianza kunitafuta baada ya kusikia nina kazi akiniomba msamaha kwa aliyonifanyia, mimi sikukubali nilimuambia aendelee na maisha yake na mimi niendelee na yangu. lakini wiki iliyopita niliamua kwenda kupima afya yangu na kukuta nimeshaambukizwa UKIMWI. Sina hakufanya,sijamuambia mtu yeyote nimebaki tu kulia peke yangu maisha yangu nayaona hayana maana tena.

***MWISHO


(WAKUBWA TU 18+) JIFUNZE UFUNDI NA UTUNDU KATIKA MAPENZI UBORESHE MAHUSIANO YAKO PAKUA APP YA UFUNDI CHUMBANI , BONYEZA HAPA KUIDOWNLOAD KWENYE SIMU YAKO

1 comment:

  1. Huu ni lazima ushuhudia usomaji na kila mtu, nipo hapa kuruhusu ulimwengu wote kujua kuhusu mtu aliyeokoa uhusiano wangu na mtu huyu mkuu anaitwa Dr IZOYA. Hakika alifanya kazi nzuri kwangu kwa kumrudisha mpenzi wangu wa zamani ambaye aliniacha na kuahidi kamwe kurudi kwangu tena. Kwa hili, nimekuja kutambua kuwa kutoa maelezo ya Dk IZOYA kwa ulimwengu utafanya mengi mazuri kwa wale walio na nyumba zilizovunja au uhusiano kwa ajili yake ili kukusaidia kurekebisha uhusiano huo uliovunjika au ndoa yako. Unaweza kumfikia kupitia anwani yake ya barua pepe: drizayaomosolution@gmail.com au kumwita moja kwa moja kwenye [+12098373537]. Kuwasiliana naye na kuona jinsi tatizo lako litatatuliwa ndani ya 24hours. Pia mtaalamu katika mambo yafuatayo ...
    (1) Unataka kurudi nyuma yako.
    (2) Unataka kukuzwa katika ofisi yako.
    (3) Unataka wanaume / wanawake kukufuate.
    (4) Unataka mtoto.
    (5) Wewe ni mjasiriamali na unataka kushinda mikataba
    (6) Unataka mume wako awe wako milele
    (7) Unahitaji msaada wa kiroho.
    (8) Umeshambuliwa na unataka kupona fedha zilizopotea.
    (9) Weka talaka
    (10) Kualika kwa mila ya fedha
    (11) Chagua uchaguzi

    ReplyDelete

Theme images by imagedepotpro. Powered by Blogger.